Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 10:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 “Mimi ni muchungaji mwema. Muchungaji mwema anatoa maisha yake kwa ajili ya kondoo wake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 10:11
25 Σταυροειδείς Αναφορές  

Daudi alipomwona yule malaika aliyekuwa anawaua watu, alimwambia, Yawe: “Mimi ndiye ninayekuwa na kosa! Mimi mwenyewe nimekosa! Hawa watu wapole hawakufanya uovu. Ninakusihi sana uniazibu mimi na jamaa ya baba yangu.”


Zaburi ya Daudi. Yawe ni muchungaji wangu; sitapungukiwa na kitu.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


Atachunga kundi lake kama muchungaji, atawakusanya wana-kondoo katika mikono yake, atawabeba kwa kifua chake, na atawaongoza polepole kondoo wanaonyonyesha.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya wachungaji wa inchi ya Israeli. Uwaambie hao wachungaji kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwenu ninyi wachungaji wa inchi ya Israeli, munaojikulisha ninyi wenyewe tu! Haiwapasi wachungaji kuwakulisha kondoo?


Nitaweka muchungaji mumoja juu yao, mufalme kama mutumishi wangu Daudi. Yeye atawakulisha na kuwa muchungaji wao.


Mutumishi wangu Daudi atakuwa mufalme wao; watakuwa na muchungaji mumoja tu. Watayafuata maagizo yangu na kushika masharti yangu.


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Lakini anayeingia kwa mulango ni muchungaji wa kondoo.


Hakuna anayekuwa na upendo mukubwa kuliko mutu anayetoa maisha yake kwa ajili ya warafiki zake.


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Na wakati Muchungaji Mukubwa atakapotokea, mutapokea taji ya utukufu isiyoweza kuharibika.


Sisi tumetambua upendo kwa njia hii: Yesu Kristo alitoa uzima wake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kutoa uzima wetu kwa ajili ya wandugu zetu.


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις