Yoane 1:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
51 Yesu akaongeza kumwambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: mutaona mbingu zimefunguka na wamalaika wa Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwenye Mwana wa Mutu!”
Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.
Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.
Mwana wa Mutu atakufa sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake, lakini ole kwa mutu yule atakayemutoa! Ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa!”
Yesu alipokwisha kubatizwa na kutoka ndani ya maji, mara moja mbingu zikafunguka, naye akamwona Roho wa Mungu akishuka kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.
Basi, ninataka mujue kwamba Mwana wa Mutu yuko na mamlaka ya kusamehe zambi hapa katika dunia.” Kwa hiyo akamwambia yule mutu mwenye kupooza: “Simama, utwae kipoyi chako na uende kwako.”
Yesu akajibu: “Mimi Ndiye! Nanyi mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”
Yesu akasema: “Kweli, kweli ninawaambia: mutu asiyeingia kwa mulango wa upango wa kondoo, lakini anapandia na kuingilia nafasi ingine, yeye ni mwizi na munyanganyi.
Yesu akamujibu: “Hakika wewe ni tayari kutoa maisha yako kwa ajili yangu? Kweli, kweli ninakuambia: mbele jogoo hajawika, utakuwa umekwisha kunikana mara tatu.”
Kweli, kweli ninawaambia: yeye anayeniamini atafanya vilevile matendo ninayofanya. Na zaidi ya ile atafanya matendo makubwa kuliko haya, kwa sababu ninakwenda kwa Baba.
Ninakuambia mambo ya kweli: wakati ulipokuwa kijana, ulijivalisha wewe mwenyewe na kwenda pahali ulipotaka. Lakini wakati utakapokuwa muzee, utanyoosha mikono yako na mutu mwingine atakuvalisha na kukupeleka pahali usipotaka.”
Basi Yesu akaongeza kuwaambia Wayuda: “Kweli, kweli, ninawaambia: Mwana hawezi kufanya kitu kwa mafikiri yake mwenyewe; anafanya tu kile ambacho anaona Baba akifanya. Na mambo yote Baba anayofanya, Mwana anayafanya vilevile.
Akaona katika maono mbingu imefunguliwa wazi, na kitu kimoja kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka, kikitelemushwa mpaka chini, kikishikwa kwenye pembe zake ine.
na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,
Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.
Ni Enoki, mutu wa kizazi cha saba tangu Adamu, ndiye aliyetabiri zamani juu yao, akisema: “Musikilize, Bwana atakuja pamoja na maelfu na maelfu ya wamalaika zake watakatifu.
Kisha nikaona mbingu imefunguka na kukatokea farasi mweupe. Yule aliyepanda juu yake anaitwa Mwaminifu na Mwenye Ukweli, kwa maana anahukumu na kupigana vita kwa haki.
Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”