“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.
Pale pale Yesu akawalazimisha wanafunzi wake waingie ndani ya chombo na kumutangulia ngambo ingine ya ziwa la Galilaya kuelekea muji Betesaida. Kwa wakati ule alibaki akiaga lile kundi la watu.
Yesu akaendelea kusema: “Ole kwako muji Korazini! Ole kwako muji Betesaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika ndani yenu ingefanyika katika muji wa Tiro na wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuonyesha masikitiko yao kwa kuvaa magunia na kujipakaa majivu, na kugeuka toka zambi zao.
Mitume waliporudia toka kuhubiri wakamwelezea Yesu mambo yote waliyofanya. Kisha akaondoka pamoja nao na kwenda kwenye nafasi ya upekee karibu na muji Betesaida.
Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Natanaeli akamwuliza: “Unanijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Filipo alipokuwa hajakuita, nilikuona wakati ulipokuwa chini ya muti wa matunda ya tini.”
Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.