Yawe anasema hivi: Simama katika kiwanja cha nyumba ya Yawe, uwatangazie watu wa miji yote ya Yuda wanaofika kuabudu katika nyumba ya Mungu, mambo yote niliyokuamuru kuwaambia, bila kuacha hata neno moja.
Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.
Basi, Baruku alisoma maneno ya Yeremia kutoka katika kile kitabu mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, katika chumba cha Gemaria mwana wa Safanu aliyekuwa katibu. Chumba hicho kilikuwa katika baraza la juu, kwenye mulango mupya wa nyumba ya Yawe.
Lakini kwa siku ya kwanza ya kufunga kula chakula, wewe utakwenda mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, usome kitabu chenye maneno ya Yawe uliyoyaandika kutoka katika kinywa changu. Utayasoma maneno hayo mbele ya watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao vilevile.
Nyuma ya mambo haya, Yeremia aliondoka Tofeti, pahali ambapo Yawe alipomutuma aende kutoa unabii, akaenda kusimama katika kiwanja cha nyumba ya Yawe, akawatangazia watu wote maneno haya:
Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.
“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.
“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!
Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.
Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa Waisraeli: Ninyi munachukia sheria ya Mungu na kupotosha mambo ya usawa.
Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli! Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.
Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.
Yawe akaniambia: Tangaza maneno hayo yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema. Uwaambie watu wayasikilize masharti ya agano hili na kuyashika.