Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yeremia 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Israeli, ulikuwa wangu wa pekee, kama malimbuko ya shamba langu. Wote waliokukula walibeba hukumu, wakipatwa na hasara. –Ni ujumbe wa Yawe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yeremia 2:3
32 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.


Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu.


Kweli! Wote waliokukasirikia, watapata haya na kufezeheka. Wote wanaopingana nawe, watakuwa wa bure na kuangamia.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.


Musikilize neno la Yawe, enyi wazao wa Yakobo. Musikilize, enyi jamaa zote za wazao wa Israeli.


Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa vilevile, na waadui zako wote watapelekwa katika uhamisho; nao wanaokukamata mateka watakamatwa mateka, nao wanaokuwinda, nitawawinda.


Watu wote waliowakuta waliwaua, na waadui zao wamesema: Sisi hatuna kosa, maana hao wamemukosea Yawe anayekuwa makao yao ya kweli; Yawe ambaye ni tegemeo la babu zao!


Muwaelezee watoto wenu jambo hili, nao wawaelezee watoto wao, na watoto wao wakielezee kizazi kinachofuata.


Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.


Kisha wanasonga mbele kama upepo, wanapita na kufanya makosa. Nguvu zao ndio mungu wao!


Lakini nimekasirikia sana mataifa ambayo yanastarehe. Nilikuwa ninayakasirikia kidogo, lakini yaliwaongezea hasara.


Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.


Ninakupa vitu vyote vizuri vinavyotokana na malimbuko ambayo Waisraeli wananitolea: mafuta safi, divai na ngano.


Donge la kwanza la unga wenye kupondwa likitolewa kwa Mungu, mikate itakuwa yake vilevile. Na kama shina la muti likitolewa kwa Mungu, matawi yatakuwa yake vilevile.


Munisalimie vilevile kanisa linalokusanyika katika nyumba yao. Munisalimie mupendwa wangu Epeneto, anayekuwa mwamini wa kwanza wa Kristo katika jimbo la Azia.


Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,


Ninyi ni watakatifu wa Yawe, Mungu wenu. Yawe amewachagua ninyi kuwa watu wake kati ya watu wote katika dunia yote.


Atawafanya ninyi kuwa taifa kubwa kuliko mataifa yote aliyoumba. Nanyi mutatetea jina lake, sifa yake na heshima yake. Ninyi mutakuwa watakatifu wake kama vile alivyosema.”


Mufanye hivyo kwa sababu ninyi mumetakaswa kwa Yawe, Mungu wenu. Kati ya watu wote katika ulimwengu aliwachagua ninyi kusudi mukuwe taifa lake mwenyewe.


Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Watu wale ndio waliojilinda katika usafi bila kujichafua kwa kulala na wanawake, nao wanamufuata Mwana-Kondoo kila fasi anapokwenda. Wamekombolewa kati ya watu wengine kusudi wakuwe wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo kama vile sadaka ya mavuno ya kwanza.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις