Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yakobo 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yakobo 3:6
62 Σταυροειδείς Αναφορές  

Halafu Abusaloma alimwambia Ahitofeli: “Unipatie shauri; tufanye nini?”


Watu wa Yuda wakawaambia watu wa Israeli: “Kwa sababu mufalme ni ndugu yetu wa karibu. Kwa nini munakasirika juu ya jambo hili? Tumekula nini wakati wowote kutoka kwake? Au yeye ametupatia zawadi yoyote?”


Abiya na jeshi lake akawapiga Waisraeli sana, akawashinda; akaua waaskari wa Israeli, elfu mia tano waliokuwa kati ya waaskari hodari sana katika Israeli.


Watu hao wanafikiri mabaya siku zote, wanaamusha ugomvi kila mara.


Unikinge na shauri baya la waovu, nayo fujo ya watu wabaya.


Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.


Mutu mwovu anapanga kutenda uovu. Maneno yake ni kama moto mukali.


mushuhuda wa uongo anayesema uongo, na mutu anayechochea fitina kati ya wandugu.


Vitakulinda mbali na mwanamuke mubaya, vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamuke mugeni.


Muangalie, Yawe mwenyewe anakuja tokea mbali! Amewaka hasira na moshi unafuka; midomo yake inaonyesha kasirani yake, maneno anayosema ni kama moto unaoteketeza.


Lakini ninyi munaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, mutembee kwa mwangaza wa moto huo, ndimi za moto muliowasha ninyi wenyewe. Kitu mutakachopata kutoka kwa Yawe ni hiki: ninyi mutalala chini na mateso makali.


Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.


Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitakuondoa katika dunia. Mwaka huuhuu utakufa, kwa sababu umewasukuma watu wamwasi Yawe.


Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa,


Wanawake hao waliwaalika Waisraeli washiriki matambiko waliyotambikia miungu yao, nao Waisraeli wakakula chakula na kuabudu miungu yao.


Mukumbuke kwamba wanawake ndio waliofuata shauri la Balamu, wakasababisha Waisraeli wamwasi Yawe kule Peori hata ugonjwa mukali ukawafikia watu wa Yawe.


Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mutu kutoka inje kinachoweza kumuchafua. Lakini kitu kinachotoka ndani yake ndicho kinachomuchafua. [


Basi akalalamika, akisema: ‘Baba Abrahamu, unisikilie huruma; umutume Lazaro achovye incha ya kidole chake katika maji, anipoleshe ulimi wangu, kwa sababu ninateswa sana katika moto huu.’


Na hata kati yenu kutatokea watu watakaotoa mafundisho ya kupotosha wengine kusudi wawavute waamini kuwafuata.


Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?


Kisha wakaleta washuhuda wa uongo waliosema: “Mutu huyu hachoki na kusema maneno ya kutukana hili hekalu letu takatifu pamoja na Sheria ya Musa!


Lakini nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto atauawa, kwa sababu atakuwa amewafundisha uasi mbele ya Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri na kuwakomboa kutoka katika utumwa, kusudi muache njia ambayo Yawe, Mungu wenu, aliwaamuru kufuata. Hivi ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.


Inafaa kuwanyamazisha watu hao kwa sababu wanapotosha jamaa nzima kwa kufundisha mambo yasiyofaa wakitafuta kupata mali kwa njia mbaya.


Vilevile si wao ndio wanaotukana jina lile nzuri mulilopewa?


Kila namna ya nyama, ndege, nyoka na samaki wanaweza kufugwa na mutu, na wamekwisha kufugwa naye.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Kwa sababu hiyo wakati nitakapokuja, nitaonyesha wazi mambo yote anayotenda akitusingizia sisi maneno mabaya. Lakini hatosheki na mambo yale, yeye mwenyewe anakataa kukaribisha wandugu wale wanaokuwa katika safari. Na wale wanaotaka kuwakaribisha, anawakataza na kuwafukuza katika kanisa.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Akawadanganya wakaaji wa dunia kwa njia ya vitambulisho alivyowezeshwa kuonyesha mbele ya yule nyama mukubwa wa kwanza. Aliwaambia watu wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule nyama aliyeumizwa kwa upanga, lakini aliendelea kuishi.


Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις