Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yakobo 2:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Lakini ninyi munawazarau wamasikini! Watajiri si ndio wale wanaowagandamiza ninyi na kuwashitaki kwenye tribinali?

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yakobo 2:6
38 Σταυροειδείς Αναφορές  

kwa sababu amewaangamiza wamasikini na kuwaachilia, amenyanganya nyumba ambazo hakuzijenga.


Muzaifu anashambuliwa na kuangushwa chini; anaangushwa kwa ukali wa mutu mwovu.


Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida; nawe uko tayari kuwasaidia siku zote. Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu, wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.


Waovu wanatesa wamasikini kwa kiburi. Mitego yao iwanase wao wenyewe!


Anajificha karibu na vijiji akivizia, amwue kwa siri mutu asiyekuwa na kosa. Yuko macho kumuvizia muzaifu;


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Unaweza kuvuruga mipango ya masikini, lakini Yawe ndiye kimbilio lake.


Anayemutesa muzaifu anamutukana Muumba wake, lakini anayemwonea huruma mukosefu anamutukuza Mungu.


Anayechekelea masikini anamutukana Muumba wake; anayefurahia hasara hatakosa kuazibiwa.


Masikini anaomba kwa unyenyekevu, lakini tajiri anajibu kwa ukali.


Anayemutesa masikini kwa kujitajirisha na anayewapa watajiri zawadi, wote wawili wataishia kuwa wamasikini.


Tajiri anamutawala masikini. Mwenye kukopesha ni mutumwa wa mwenye kukopeshwa.


Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Umetoboa vichwa vya wakubwa wao kwa mikuki yao wenyewe, waliotufikia kama zoruba kututawanya, wakijivuna kwa kuwameza wamasikini kwa siri.


Musiwatese wajane, wayatima, wageni au wamasikini; musipange kutendeana mabaya ndani ya mioyo yenu.


Yesu akajibu: “Mimi sina pepo, lakini ninamuheshimu Baba yangu, nanyi munanikosea heshima.


Lakini Wayuda wakawashawishi wakubwa wa muji pamoja na wanawake wamoja wenye heshima, walioabudu Mungu. Wakawatesa Paulo na Barnaba hata wakawafukuza toka katika inchi yao.


Kwa kuwa hawakuwapata, wakamupeleka Yasoni pamoja na wandugu waamini wengine mbele ya wakubwa wa muji. Wakalalamika wakisema: “Watu hawa walifanya fujo fasi zote na sasa wamefika huku.


Katika nyakati Galio alipokuwa liwali wa jimbo la Akaya, Wayuda wakamufanyia Paulo shauri baya kwa nia moja, wakamukamata na kumupeleka mbele ya tribinali,


Lakini Saulo aliendelea kuteketeza kanisa, akiingia nyumba kwa nyumba, na kuwakamata waamini, wanaume na wanawake, na kwenda kuwatupa katika kifungo.


Basi, ninyi hamuna nyumba munamoweza kukulia na kukunywea? Au munazarau kanisa la Mungu na munataka kuwapatisha haya wale wasiokuwa na kitu? Munataka niwaambie ninyi nini? Inafaa niwasifu? Hapana, siwezi kuwasifu hata kidogo juu ya jambo hilo!


Halafu munaonyesha heshima kwa yule anayevaa vizuri na kumwambia: “Ikaa hapa kwenye nafasi nzuri.” Lakini munamwambia yule masikini: “We! Simama pale, au uikae hapa chini kwenye nafasi ya kuwekea miguu yangu.”


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


Mumewahukumu na kuwaua wenye haki, nao hawakupingana nanyi.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις