7 Mutu wa namna hiyo asizani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Bwana,
Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.
Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.
Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.
Lakini inafaa aombe kwa imani pasipo kuwa na mashaka. Kwa maana mutu anayekuwa na mashaka anafanana na zoruba katika bahari inayosukumwa na upepo na kutupa maji huku na huko.
kwa sababu ni mutu wa nia mbili, na mwenye kugeukageuka katika mwenendo wake.
Wakati munapoomba, hamupati kitu kwa sababu munaomba kwa nia mbaya, kwa maana munataka vitu kusudi mutimize tu tamaa zenu.