Walawi 7:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200218 Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani inakuliwa kwa siku ya tatu, mutu aliyeitoa hatakubaliwa, wala hiyo sadaka haitapokelewa kwa faida yake. Nyama hiyo ni chukizo na mutu atakayeikula atabeba lazima ya uovu wake. Δείτε το κεφάλαιο |
Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.
Kama mwanaume yeyote akimwoa dada yake, binti ya baba yake au mama yake na binti huyo akakubaliana na mwanaume huyo ambaye ni kaka yake, na kulala naye, hilo ni chukizo. Wanapaswa kutengwa na watu wao maana wamefanya jambo la haya. Huyo mwanaume atabeba lazima ya uovu wake, maana amelala na dada yake.