Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Walawi 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Lakini kama hawezi kutoa mwana-kondoo wa sadaka ya kosa kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi atamuletea Yawe hua wawili au vitoto viwili vya njiwa, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Walawi 5:7
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, ikuwe amepata mutoto mwanaume au mwanamuke, atamuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano mwana-kondoo wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kitoto cha njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya zambi.


Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


Kisha kuhani atatwaa mumoja wa wale hua au njiwa wawili kadiri mutu yule anavyoweza kuleta.


Hua atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Pamoja na hao, atatoa sadaka ya vyakula. Kuhani atamufanyia mutu yule ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.


Kuhani atatoa mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Hivyo kuhani atamufanyia huyo mwanamuke ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa damu.


Atatwaa kutoka watu wa Israeli beberu wawili kwa ajili ya sadaka ya zambi na kondoo dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Lakini ikiwa mutu huyu ni masikini na hawezi kulipa malipo yake, basi, mutu yule atapelekwa kwa kuhani. Kuhani atapima bei yake kulingana na uwezo wa huyo aliyefanya kiapo.


Ikiwa hawezi kutoa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kama vile sadaka yake kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi, ataleta unga kilo moja. Lakini hatautia mafuta wala ubani maana ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Hii ndiyo sheria ya ibada kuelekea sadaka kwa ajili ya kosa. Sadaka hiyo ni takatifu kabisa.


Uwaambie Waisraeli watwae beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi, na mwana-ngombe mumoja na mwana-kondoo mumoja wote wa umri wa mwaka mumoja na wasiokuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,


Uwaambie Waisraeli kwamba: Mutu yeyote, mwanaume au mwanamuke, akimukosea mwenzake, yeye anatenda zambi mbaya mbele ya Yawe.


Katika siku ya nane atapeleka hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kwa kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano.


Kuhani atamutoa mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, naye atamufanyia ibada ya upatanisho, kwa sababu alitenda zambi kwa sababu ya maiti. Siku hiyohiyo atatakasa kichwa chake


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


Yesu akaingia ndani ya hekalu, naye akawafukuza watu wote waliokuwa wakiuzishia na kununulia vitu vyao ndani yake. Akapindua meza za wale waliobadilisha feza na viti vya wachuuzi wa njiwa.


Yesu alipokwisha kubatizwa na kutoka ndani ya maji, mara moja mbingu zikafunguka, naye akamwona Roho wa Mungu akishuka kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Wakatoa vilevile sadaka sawa vile inavyoagizwa katika Sheria ile: “Hua wawili au vitoto viwili vya njiwa.”


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις