Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Walawi 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kama sadaka hiyo ya amani unayomutolea Yawe ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au dike asiyekuwa na kilema.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Walawi 3:6
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Makundi ya nyama wa inchi ya Kedari yatakusanyika kwako, utaweza kuwatumia kondoo dume wa Nebayoti; utatoa sadaka inayokubaliwa kwenye mazabahu ya Mungu, naye ataitukuza nyumba yake tukufu.


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Uwaambie Waisraeli kwamba kama mutu anapenda kumutolea Yawe sadaka ya nyama, nyama huyo atamuchagua kutoka kundi lake la ngombe, kondoo au mbuzi.


Munaponitolea mimi Yawe sadaka za amani, mutanitolea kama vile inavyotakiwa kusudi mupate kukubaliwa.


Inakatazwa kutoa chochote kinachokuwa na kilema maana hakitakubaliwa kwa faida yenu.


Mutatoa beberu mumoja wa sadaka kwa ajili ya zambi na wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka za amani.


Toa litre moja ya divai kama sadaka ya kinywaji kwa kila mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa kwa moto au sadaka ingine.


na kumutolea Yawe zawadi zake: mwana-kondoo dume mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; mwana-kondoo dike mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya zambi; na kondoo dume mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya amani.


“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις