Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Walawi 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Walawi 3:1
29 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Akamwomba Yawe, naye akakubali maombi yake kwa kuleta moto kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka kwenye mazabahu.


Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.


Kisha akatuma vijana wa watu wa Israeli wamutolee Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na kumuchinjia sadaka za amani za ngombe.


Hivyo siku zote Waisraeli watatwaa sehemu hizo kutoka katika sadaka zao za amani wanazonitolea mimi Yawe na kumupa Haruni na wana wake. Hiyo ni sadaka yao kwa Yawe.


“Ilinipasa kutoa sadaka zangu; leo hii nimekamilisha naziri yangu.


Kisha siku hizo saba, tokea siku ya nane na kuendelea, makuhani watatoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani. Nami nitawakubali. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Watatoa kondoo mumoja kwa kila kundi la kondoo mia mbili katika jamaa za Waisraeli. Wataleta sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani, kusudi wapate kufanyiwa upatanisho. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Agizo hili linalazimisha Waisraeli kuletea Yawe nyama ambao wanawachinja katika mashamba. Wataleta nyama wale kwa kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano, naye atawachinja na kumutolea Yawe sadaka za amani.


Kama sadaka hiyo ya amani unayomutolea Yawe ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au dike asiyekuwa na kilema.


Halafu Haruni akamuchinja vilevile ngombe dume na yule kondoo dume wa sadaka za amani kwa ajili ya watu. Wana wake wakamuletea damu ambayo aliinyunyizia mazabahu pande zote.


ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya amani, wamutolee Yawe sadaka pamoja na sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa maana leo Yawe atawatokea.


Hata mukinitolea sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na za vyakula, mimi sitakubali kuzipokea; na sadaka zenu za amani za nyama wanono mimi sitaziangalia kabisa.


Alaaniwe mutu yeyote anayenidanganya, ambaye anaahidi kwa kiapo kunitolea sadaka ya nyama safi kutoka kundi lake, lakini ananitolea sadaka ya nyama mwenye kilema. Mimi ni mufalme mukubwa, na watu wa mataifa yote wananiogopa. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Munaponitolea sadaka ya nyama anayekuwa kipofu, au kilema, au mugonjwa, huo si uovu? Mutawala atapendezwa au kukutendea mema ukimupa zawadi ya nyama kama yule? –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Wakati mutakapomutolea Yawe mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au sadaka kwa kutimiza kiapo au kwa ajili ya sadaka za amani,


na kumutolea Yawe zawadi zake: mwana-kondoo dume mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; mwana-kondoo dike mumoja wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya zambi; na kondoo dume mumoja asiyekuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya amani.


Hapo, mutatoa sadaka za kuteketezwa, nyama na damu, kwenye mazabahu ya Yawe, Mungu wenu. Damu ya nyama mutainyunyiza kwenye mazabahu ya Yawe Mungu wenu, lakini munaruhusiwa kula nyama.


Kwa njia ya Mwana wake alitaka kupatanisha ulimwengu muzima naye. Kwa njia ya damu ya Mwana wake iliyomwangika juu ya musalaba, Mungu ameleta amani, hivi akapatanisha vitu vyote naye mwenyewe, vinavyokuwa katika dunia na katika mbingu.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Watu wote wa jeshi la Waisraeli wakaenda Beteli. Wakaikaa kule mbele ya Yawe wakiomboleza na kufunga mpaka magaribi. Wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.


Kesho yake watu wakaamuka mapema, wakajenga mazabahu, wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις