Hakuna sehemu yoyote ya eneo hilo itakayouzishwa au kutolewa kwa mutu yeyote, kwa sababu eneo hilo ni takatifu kwa Yawe; nalo ni bora kuliko yote katika inchi.
Hairuhusiwi kumubadilisha nyama huyo na mwingine yeyote, muzuri kwa mubaya au mubaya kwa muzuri. Kama akimubadilisha na nyama mwingine, wote wawili watakuwa watakatifu.
Lakini ikiwa mutu huyu ni masikini na hawezi kulipa malipo yake, basi, mutu yule atapelekwa kwa kuhani. Kuhani atapima bei yake kulingana na uwezo wa huyo aliyefanya kiapo.
Kama mutu yeyote akikosa kwa kutenda zambi bila kujua juu ya kutokutoa vitu vitakatifu Yawe anavyotolewa, atamuletea kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake. Wewe utapima bei yake kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya kosa.
Lakini ninyi munasema kwamba mutu akiwa na kitu ambacho angeweza kuwasaidia baba yake au mama yake, lakini akimwambia kwamba amekitoa sadaka kwa Mungu,