Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Walawi 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mumoja chetezo chake, wakaweka moto na ubani, wakamutolea Yawe moto usioruhusiwa, ambao haukulingana na agizo la Yawe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Walawi 10:1
38 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mara moja, Yawe akashusha moto, ukaiteketeza sadaka ile ya kuteketezwa, kuni, mawe na mavumbi, na kuyakausha maji yote katika mufereji.


Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Yawe akamwambia Musa: Mukuje kwangu, wewe Haruni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee makumi saba wa Israeli, muniabudu kwa mbali.


Kisha Musa, Haruni, Nadabu na Abihu na wazee makumi saba wa Israeli wakapanda juu ya mulima,


Utaitengenezea vyombo vyake: vyungu vya kuwekea majivu, majembe, na mabeseni, na kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote utavitengeneza kwa shaba.


Nawe Musa umulete kwangu Haruni ndugu yako, pamoja na wana wake: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari. Utawachagua kati ya Waisraeli, kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


mafuta ya kupakaa na ubani wenye harufu nzuri kwa ajili ya Pahali Patakatifu. Vitu hivyo vyote vitatengenezwa kulingana kabisa na jinsi nilivyokuamuru.


Akatengeneza mafuta matakatifu ya kupakaa na ubani safi wenye harufu nzuri uliochanganywa vizuri kama manukato.


Akatengeneza vilevile vyombo vyote kwa ajili ya mazabahu: vyungu, majembe, mabeseni, kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote akavitengeneza kwa shaba.


na kufukiza ubani wenye harufu nzuri juu yake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Haruni alimwoa Eliseba, binti ya Aminadabu, dada ya Nasoni; naye akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.


Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Wale mainzi wakatoweka kutoka kwa mufalme wa Misri, wakubwa wake na watu wake, wala hakukubaki hata mumoja.


wanamujengea mungu Bali mazabahu, kwa kusudi la kuwachoma wana wao kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya mungu yule. Mimi sikuwaamuru hata kidogo kufanya vile, wala halikunifikia katika roho.


Walimujengea mungu Bali mazabahu katika bonde la Mwana wa Hinomu, kusudi wamutolee mungu Moleki wana wao na wabinti zao, ingawa sikuwaamuru wala sikufikiria kwamba wangefanya hivyo. Wakasukuma watu wa Yuda watende zambi.


Kisha, wanaume wote waliojua kwamba wake wao walikuwa wameifukizia miungu mingine ubani, na wanawake wote waliokuwa hapo, kusanyiko kubwa la watu pamoja na Waisraeli waliokuwa wanakaa Patro katika inchi ya Misri walimujibu Yeremia:


Kwa nini munanichochea nikasirike kwa kuabudu sanamu mulizojitengenezea wenyewe na kuifukizia ubani miungu mingine katika inchi ya Misri ambamo mumekuja kuishi? Munataka kuangamizwa na kuwa laana na kuchekelewa mbele ya mataifa yote katika dunia?


Wamejenga mazabahu inayoitwa “Tofeti” huko kwenye bonde la Mwana wa Hinomu, kwa kuwatolea wana na wabinti kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Mimi sikukuwa nimewaamuru kufanya jambo hilo, wala halikunifikia katika mafikiri.


Yawe akazungumuza na Musa, kisha kufa kwa wana wawili wa Haruni wakati ule walipomukaribia.


Halafu atatwaa chetezo na kutwaa makaa toka kwenye mazabahu mbele ya Yawe na mikono miwili ya ubani uliosagwa vizuri sana na atauleta ndani ya pazia.


Kwa hiyo, makuhani washike agizo langu, kusudi wasifanye zambi na kuuawa. Mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


Nadabu na Abihu walikufa walipomutolea Yawe sadaka ya moto usiofaa.


Musiache ukoo wa jamaa za Kohati kati ya Walawi uangamizwe.


naye amekwenda na kutumikia miungu mingine na kuiabudu, akiabudu jua, mwezi au vitu vingine vya mbinguni nisivyoagiza,


Musiongeze chochote katika amri ninazowapa, wala musipunguze kitu. Mushike amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa.


Ndani ya chumba kile kulikuwa chombo cha kufukizia ubani, kilichotengenezwa na zahabu. Na kulikuwa vilevile Sanduku la Agano lililopakaliwa zahabu pande zote. Ndani ya sanduku lile kulikuwa kopo la zahabu lenye mana, na fimbo ya Haruni iliyoota vichipukizi juu yake. Kulikuwa vilevile vibao vya mawe vyenye Maandiko ya Agano la Mungu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις