Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Walawi 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kisha, atamuchinja huyo ngombe mbele ya Yawe. Nao makuhani wazao wa Haruni wataichukua damu na kuinyunyizia mazabahu inayokuwa kwenye mulango wa hema la mukutano, pande zake zote.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Walawi 1:5
25 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakachinja mwana-kondoo wa Pasaka, nao makuhani wakanyunyiza damu waliyopokea kwa mikono yao nao Walawi wakachuna nyama.


na kumuchinja mbele ya Yawe, kwenye mulango wa hema la mukutano.


Nawe utamuchinja na damu yake utairushia juu ya mazabahu pande zake zote.


Ile mazabahu ya kuteketezea sadaka utaiweka mbele ya mulango wa hema takatifu la mukutano.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Bwana wetu Yawe akaniambia. Wewe mwanadamu! Yawe anasema hivi: Wakati mazabahu itakapojengwa utaitakasa, kwa kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake na kuinyunyizia damu ya nyama waliotolewa.


Atamuchinjia upande wa kaskazini wa mazabahu, mbele ya Yawe, hao makuhani wazao wa Haruni watainyunyizia mazabahu damu pande zake zote.


Kuhani ataleta ndege huyo kwenye mazabahu, atakongonyoa kichwa chake na kukiteketeza juu ya mazabahu. Damu yake itanyunyiziwa kwenye ubavu wa mazabahu.


Halafu atachinja yule beberu wa sadaka ya zambi kwa ajili ya watu wote. Damu ya mbuzi huyo ataileta ndani ya Pahali Patakatifu Sana na kufanya kama vile alivyofanya na damu ya yule ngombe dume; atainyunyiza juu ya kiti cha rehema, upande wake wa mbele.


Itakuwa hivyo kwa sababu uzima wa kiumbe uko katika damu. Nimewaagiza kutolea damu kwenye mazabahu kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya roho zenu, kwa sababu damu inafanya upatanisho, nao uzima uko katika damu.


akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.


Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja kwenye mulango wa hema la mukutano. Hao makuhani wazao wa Haruni watainyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.


akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Makuhani wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.


Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mbuzi huyo wa sadaka ya kuondoa zambi, na kumuchinjia pahali wanapochinjia nyama wa sadaka za kuteketezwa.


Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mwana-kondoo huyo wa sadaka kwa ajili ya zambi na kumuchinjia pahali pale wanapochinjia nyama wa sadaka za kuteketezwa.


Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Nimwendee Yawe na kitu gani, nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu? Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto, nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?


Lakini wazaliwa wa kwanza wa ngombe, kondoo au mbuzi wasikombolewe; hao ni watakatifu. Damu yao utainyunyizia mazabahu na mafuta yao utayateketeza kuwa sadaka ya kuteketezwa ambayo ni harufu nzuri inayonipendeza mimi Yawe.


Kila kuhani anasimama mbele ya Mungu kila siku kwa kufanya ibada na kutoa sadaka za namna moja mara nyingi zisizoweza hata kidogo kuondoa zambi.


Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.


Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.


Walipokwisha kuchinja yule ngombe dume, walimupeleka mutoto kwa kuhani Eli.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις