Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Walawi 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akamwita Musa na kuongea naye katika hema la mukutano, akamwambia:

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Walawi 1:1
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Alitolea sadaka yake ya kuteketezwa, ya ngano, na ya kinywaji, akanyunyiza damu ya sadaka ya amani.


Sadaka za kuteketeza walizoleta kwa jumla zilikuwa ngombe dume makumi saba, kondoo dume mia moja na wana-kondoo mia mbili. Zote hizo zilikuwa sadaka za kuteketeza kwa ajili ya Yawe.


Basi, Musa akapanda juu kwenye mulima kwa Mungu. Halafu Yawe akamwita Musa kutoka kule juu ya mulima, akamwambia: “Hivi ndivyo utakavyowaambia wazao wa Yakobo, wale Waisraeli:


Yawe akamwambia Musa: Kuja kwangu juu kwenye mulima, ungoje kule. Mimi nitakupa vibao vya mawe vyenye sheria na amri nilizoandika kwa ajili ya kuwafundisha Waisraeli.


Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.


Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa siku zote, kizazi kwa kizazi, mbele yangu mimi Yawe, mbele ya mulango wa hema la mukutano ambapo mimi nitakutana nanyi na kuongea nanyi.


Yawe alipoona kwamba Musa amegeuka kwa kuangalia kichaka, akamwita pale kutoka kichaka: “Musa! Musa!” Musa akaitika: “Niko hapa. Ninasikiliza!”


Musa alikuwa na desturi ya kuchukua lile hema na kulisimika inje ya kambi. Hema hilo alilipa jina, hema la mukutano. Mutu yeyote aliyetaka shauri kwa Yawe alikwenda kwenye hema la mukutano inje ya kambi.


Basi, kazi yote ya hema la mukutano ikamalizika. Waisraeli walifanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


akaweka pale kwenye mulango wa hema takatifu mazabahu ya sadaka za kuteketezwa, akatolea juu yake sadaka ya kuteketezwa kwa moto na sadaka ya ngano, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Yawe akamupa Musa amri hizi juu ya mulima Sinai siku ile alipowaamuru Waisraeli wamuletee sadaka zao, kule katika jangwa la Sinai.


Kisha akaleta mbele ile sadaka ya kuteketezwa akatolea sadaka hiyo kulingana na agizo.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:


Wakati Musa alipoingia ndani ya hema la mukutano kwa kuongea na Yawe, akasikia sauti kutoka upande wa juu wa kiti cha rehema, kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano, kutoka kati ya wale makerubi.


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Mutamujengea Yawe, Mungu wenu, mazabahu kwa mawe yasiyochongwa. Juu ya mazabahu hiyo mutamutolea Yawe, Mungu wenu, sadaka za kuteketezwa.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις