Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Waebrania 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Jambo la lazima sana katika maneno tunayosema sasa ni hili. Tuko na Mukubwa wa namna ile, anayeikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mwenyezi Mungu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Waebrania 8:1
21 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Mwangaza muzuri unatokea upande wa kaskazini; Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha.


Umusifu Yawe, ee nafsi yangu! Ee Yawe, Mungu wangu, wewe ni mukubwa kabisa! Umevaa utukufu na mamlaka.


Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


kusudi kila mutu ajue matendo yako makubwa, na mamlaka ya ufalme wako wenye utukufu.


Alikuomba maisha, nawe ukamupatia; ulimupatia siku nyingi milele na milele.


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Bwana Yesu alipokwisha kusema nao maneno hayo, akanyanyuliwa juu kwenda mbinguni na kuikaa kwa upande wa kuume wa Mungu.


Mimi ni mujumbe wa Habari ile Njema, ijapokuwa sasa ninakuwa katika kifungo. Basi muniombee kusudi nipate kusema kwa uhodari, sawa inavyonipasa kusema.


Kwa kuwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, mutafute mambo yanayokuwa juu, pahali Kristo anapoikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.


Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu, mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Lakini Kristo yeye alitoa sadaka moja tu inayofaa kwa milele kwa ajili ya usamehe wa zambi. Na kisha akaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Basi, kwa kuwa tuko na Kuhani Mukubwa zaidi aliyeingia mbinguni, ndiye Yesu Mwana wa Mungu, tushikamane sana na imani tunayotangaza.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις