Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Waebrania 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi musigeuke kuwa wavivu, lakini mufuate mufano wa wale wanaoamini na kuvumilia. Kwa njia hiyo wanapokea yale Mungu aliyoahidi kuwapa.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Waebrania 6:12
36 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kuwa na bidii kutamupa mutu cheo, lakini uvivu utamufanya mutumwa.


Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.


Njia ya muvivu inajaa miiba, lakini njia ya mutu wa usawa ni wazi kama barabara kubwa.


Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.


Kwa hiyo utafuata mufano wa watu wazuri, na kufuata mienendo ya wenye haki.


Kama vile mulango unavyozunguka kwenye vyuma vya kuukamatia, ndivyo muvivu anavyogeuka juu ya kitanda chake.


Anayepotosha mutu wa usawa katika njia mbaya, ataanguka katika shimo lake mwenyewe. Wakamilifu watarizi mazuri.


Ewe unayependeza kuliko wanawake wote; kama haujui, fanya hivi: ufuate nafasi kondoo walipopita; basi, uwakulishie mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ ” Yesu akaendelea kuwaambia: “Mungu si Mungu wa waliokufa, lakini ni Mungu wa wanaokuwa wazima.”


Naye bwana wake akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya na muvivu! Ulijua kama ninavuna nafasi nisipopanda, na kukusanya nafasi nisiposambaza.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Musikuwe wavivu katika kazi lakini mukuwe na bidii, mukimutumikia Bwana kwa juhudi.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Vilevile yeye ni baba ya wale wanaotahiriwa, si kwa sababu wametahiriwa tu, lakini kwa sababu wanafuata vilevile njia ile ile ya imani ambayo babu yetu Abrahamu alifuata alipokuwa hajatahiriwa.


Kwa maana tunakumbuka mbele ya Mungu Baba yetu namna munavyotumika kwa imani na munavyojisumbua na kazi kwa ajili ya upendo wenu. Vilevile tunakumbuka namna tumaini lenu katika Yesu Kristo linavyokuwa imara.


Kufuatana na ile, sisi tunajivuna kwa ajili yenu katika makanisa ya Mungu kwa sababu ya uvumilivu wenu na imani munayokuwa nayo katika mateso na taabu munazopata.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Kwa njia ya imani hawa walishinda inchi za wafalme, walitenda mambo ya haki na kupata yale Mungu aliyowaahidi. Walifunga vinywa vya simba,


Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa.


Muwakumbuke waongozi wenu waliowatangazia neno la Mungu. Muangalie vizuri namna walivyoishi na kufa. Mufuate imani yao.


Tuna maneno mengi ya kusema juu ya jambo hili, lakini ni vigumu kuyaeleza kwenu kwa sababu ninyi mumekuwa na masikio magumu.


Hivi kisha kungojea kwa uvumilivu, Abrahamu akapokea yale Mungu aliyomwahidi.


kwa maana munajua kwamba kupimwa kwa imani yenu kunawaletea uvumilivu.


Kwa hiyo wandugu zangu, kufuatana na vile mulivyochaguliwa na kuitwa na Mungu, mufanye nguvu zaidi kwa kukamilika katika njia ile. Mukitenda mambo yale hamutaanguka hata kidogo.


Na Kristo yeye mwenyewe alituahidi sisi uzima wa milele.


Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις