Waebrania 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20025 Musa alikuwa mutumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, kusudi ashuhudie maneno ambayo Mungu angesema nyuma. Δείτε το κεφάλαιο |
Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.
Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”
Mutawasaidia mpaka Yawe atakapowapa wandugu zenu vilevile pahali pa kupumzika, kama vile alivyowapa ninyi, nao vilevile warizi inchi ambayo wanapewa na Yawe, Mungu wenu. Kisha mutarudi katika inchi ambayo ni mali yenu na kuirizi, inchi ambayo mulipewa na Musa, mutumishi wa Yawe, ngambo ya muto Yordani.”
kama vile Musa mutumishi wa Yawe alivyowaagiza Waisraeli, kadiri ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa kwamba itakuwa mazabahu iliyojengwa kwa mawe ambayo hayakuchongwa, wala kuguswa na chombo chochote cha chuma. Juu ya mazabahu hiyo wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.
Waisraeli wote pamoja na viongozi wao, wazee na waamuzi na wageni wote waliokuwa kati yao, wakasimama kila upande kuelekeana na Sanduku la Agano mbele ya makuhani Walawi waliokuwa wamelibeba Sanduku la Agano la Yawe. Nusu yao wakasimama mbele ya mulima Gerizimu na nusu nyingine wakasimama mbele ya mulima Ebali, kama vile Musa, mutumishi wa Yawe alivyoagiza pale mbele juu ya kubarikiwa kwa Waisraeli.