Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Waebrania 13:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Waebrania 13:20
53 Σταυροειδείς Αναφορές  

Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


Alimusimamishia Yakobo ahadi yake, akamuhakikishia agano hilo la milele.


Nguvu za Mungu zilikuwa zikifanya kazi katika Yuda, zikitia moyo wa kutii amri za mufalme na wakubwa wake kadiri ya maagizo ya Yawe.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni muchungaji wangu; sitapungukiwa na kitu.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


Musa akatwaa ile damu na kuwanyunyizia watu, akisema: Hii ndiyo damu ya agano ambalo Yawe amefanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.


Atachunga kundi lake kama muchungaji, atawakusanya wana-kondoo katika mikono yake, atawabeba kwa kifua chake, na atawaongoza polepole kondoo wanaonyonyesha.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


Nitaweka muchungaji mumoja juu yao, mufalme kama mutumishi wangu Daudi. Yeye atawakulisha na kuwa muchungaji wao.


Mutumishi wangu Daudi atakuwa mufalme wao; watakuwa na muchungaji mumoja tu. Watayafuata maagizo yangu na kushika masharti yangu.


Nitafanya nao agano la amani, nalo litakuwa agano la milele. Nitawabariki na kuwafanya wakuwe wengi, nami nitaweka hekalu langu kati yao milele.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya agano langu pamoja nanyi, agano lililokamilishwa kwa njia ya damu, nitawakomboa wafungwa wenu wanaokuwa kama wamefungwa katika shimo tupu.


kwa maana hii ni damu yangu inayomwangika kwa ajili ya wengi kusudi wasamehewe zambi. Nayo damu hii inahakikisha agano la Mungu.


Na Yesu akawaambia: “Hii ni damu yangu; damu inayomwangika kwa ajili ya watu wengi kwa kuhakikisha agano la Mungu.


Vilevile kisha kula akatwaa kikombe na kuwapa akisema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu.]


“Mimi ni muchungaji mwema. Muchungaji mwema anatoa maisha yake kwa ajili ya kondoo wake.


Mimi ni muchungaji mwema. Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua,


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Lakini Mungu alimufufua, akimufungua toka vifungo vya lufu, kwa sababu haikuwezekana afungwe na lufu.


“Mungu alimufufua huyo Yesu, na sisi wote tuko washuhuda wa jambo hili.


Halafu mukamwua yule anayekuwa asili ya uzima, lakini Mungu amemufufua. Na sisi ni washuhuda wa jambo hilo.


Kwa hiyo, ninyi wote pamoja na Waisraeli wote mujue vizuri kwamba mutu huyu anayesimama mbele yenu akiwa muzima kabisa, ni kwa uwezo wa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, yule muliyemutundika juu ya musalaba, lakini Mungu amemufufua.


Mungu wa babu zetu alimufufua Yesu, yule ninyi muliyemwua kwa kumutundika juu ya musalaba.


Wala usijiulize: “Ni nani atakayeshuka katika kuzimu?” (maana yake kumupandisha Kristo toka kule kwenye wafu).


Basi Mungu anayeleta amani akuwe pamoja nanyi wote. Amina!


Mungu, anayeleta amani, atamupondaponda sasa hivi Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikuwe pamoja nanyi.


Na kama Roho wa Mungu aliyemufufua Yesu anakaa ndani yenu, basi huyo aliyemufufua Kristo ataupatia mwili wenu unaokuwa wa kufa uzima kwa njia ya Roho wake anayekaa ndani yenu.


kwa maana Mungu hataki sisi tuishi katika fujo, lakini katika amani. Sawa vile inavyokuwa desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu,


Na zaidi ya hii, sisi tumeonekana kuwa washuhuda wa uongo mbele ya Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kuwa Mungu amemufufua Kristo, ingawa hakumufufua, ikiwa kweli wafu hawafufuki.


Mungu aliyemufufua Bwana Yesu atatufufua nasi vilevile kwa uwezo wake.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Tunajua kwamba Mungu aliyemufufua Bwana Yesu atatufufua sisi vilevile pamoja na Yesu. Yeye atatufikisha pamoja nanyi mbele ya Yesu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.


Alifanya vile wakati alipomufufua Kristo na kumwikalisha na mamlaka kwa kuume kwake mbinguni.


Mushike mambo yote muliyojifunza na kupokea toka kwangu, nayo yote muliyosikia na kuona kwangu. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.


Kwa maana mumezikwa pamoja na Kristo kwa njia ya ubatizo, nanyi mumefufuliwa vilevile pamoja naye, kwa sababu mumeamini uwezo wa Mungu, aliyemufufua.


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Bwana wa amani mwenyewe awape amani siku zote na kwa njia zote. Bwana akuwe pamoja nanyi wote.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Naye akasema: “Hii ndiyo damu inayohakikisha agano lile Mungu analowaamuru kutii.”


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Na wakati Muchungaji Mukubwa atakapotokea, mutapokea taji ya utukufu isiyoweza kuharibika.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις