Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Waebrania 11:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Waebrania 11:9
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha Abramu akaondoka, akaelekea kwenye mulima upande wa mashariki ya Beteli akapiga hema kati ya muji wa Beteli, upande wa magaribi, na muji wa Ai upande wa mashariki. Pale vilevile akamujengea Yawe mazabahu na kumwomba kwa jina lake.


Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Akaendelea kusafiri toka eneo la Negebu mpaka Beteli. Alifika pahali alipokuwa amepiga kambi ya hema mara ya kwanza kati ya Beteli na Ai,


Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


Abrahamu akarudi haraka ndani ya hema akamwambia Sara: “Tayarisha haraka vipimo vitatu vya unga bora, uuponde, uchome mikate.”


Wale wageni wakamwuliza: “Muke wako Sara yuko wapi?” Abrahamu akawajibu: “Yuko ndani ya hema.”


Abrahamu alikaa katika inchi ya Wafilistini muda murefu.


“Mimi ninaishi kama mugeni kati yenu. Munipatie sehemu ya udongo ya kaburi, kusudi nipate kumuzika marehemu muke wangu.”


Watoto hao wakakomaa. Esau alikuwa mwindaji hodari. Alipenda maisha ya pori. Yakobo alikuwa mutu mutulivu. Alipenda maisha ya nyumba.


Akubariki wewe pamoja na wazao wako kama alivyomubariki Abrahamu, upate kurizi inchi ambamo unakaa kama mugeni, inchi ambayo Mungu alimupa Abrahamu!”


Basi, Labani akamufikia Yakobo. Wakati ule Yakobo alikuwa amepiga kambi yake kwenye milima. Labani naye, pamoja na wandugu zake, akapiga kambi yake kwenye milima ya Gileadi.


Yakobo akaondoka akakwenda Mamure kwa baba yake Isaka, kule Kiriati-Arba ni kusema Hebroni, pahali ambapo Abrahamu na Isaka walikaa kama wageni.


Alifanya hivyo kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi hata wasiweze kuishi pamoja. Inchi walimokaa kama wageni haikuweza kuwatoshelea kwa sababu ya wingi wa nyama wao.


Yakobo akamujibu: “Umri niliojaliwa kama musafiri ni miaka mia moja na makumi tatu. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia hesabu ya miaka wazee wangu waliyoishi kama wasafiri.”


Watu wa Mungu walikuwa wachache tu, tena walikuwa wageni katika inchi ya Kanana.


Musijenge nyumba, musilime mashamba, wala musikuwe na shamba la mizabibu. Lakini mutaishi katika mahema siku zote za maisha yenu, kusudi mupate kuishi siku nyingi katika inchi munamoishi kama wageni.


Naye Mungu, kwa sababu alitaka kuonyesha wazi kwa wale watakaopokea ahadi kwamba yeye hawezi kubadilisha shauri lake hata kidogo, akaihakikisha kwa kiapo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις