Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Waebrania 11:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Kwa njia ya imani wazazi wa Musa walimuficha kwa muda wa miezi mitatu nyuma ya kuzaliwa kwake. Kwa sababu waliona kwamba alikuwa mutoto mwenye sura nzuri, wala hawakuogopa amri ya mufalme.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Waebrania 11:23
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe yuko nami, siogopi kitu; mwanadamu ataweza kunifanya nini?


Ee Mungu Mukubwa, wakati ninapoogopa, mimi ninakutumainia wewe.


“Munapofanya kazi ya kuzalisha wanawake Waebrania, ikiwa mutoto anayezaliwa ni mwanaume, mumwue. Ikiwa ni mwanamuke, mumwache aishi.”


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Hivyo, mufalme Dario akatia sahihi kwenye sheria hiyo.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Na katika siku zile Musa akazaliwa, naye alikuwa mutoto muzuri sana. Alilelewa muda wa miezi mitatu katika nyumba ya baba yake.


Kwa sababu hii tunaweza kusema kwa uhodari: “Bwana ndiye musaidizi wangu; sitaogopa kitu. Mwanadamu ataweza kunifanya nini?”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις