Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Waebrania 10:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Yeye ametufungulia njia mupya ya uzima, inayopitia katika pazia, maana yake mwili wake mwenyewe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Waebrania 10:20
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Halafu atachinja yule beberu wa sadaka ya zambi kwa ajili ya watu wote. Damu ya mbuzi huyo ataileta ndani ya Pahali Patakatifu Sana na kufanya kama vile alivyofanya na damu ya yule ngombe dume; atainyunyiza juu ya kiti cha rehema, upande wake wa mbele.


Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.


Lakini asilikaribie lile pazia wala ile mazabahu maana ana kilema, asipate kuchafua Pahali Patakatifu, kwa sababu mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.


Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,


Basi pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.


Basi Yesu akaongeza kusema: “Kweli, kweli ninawaambia: mimi ni mulango wa upango wa kondoo.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Yeye aliondoa Sheria ya Kiyuda pamoja na amri zake na maagizo yake akifanya watu wa jamii hizi mbili kuwa watu wa taifa moja jipya katika kuungana naye na kuleta amani.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Tumaini hili linasimamisha imara na kulinda mioyo yetu kama vile nanga inavyosimamisha mashua imara. Nalo linapita katika pazia na kuingia katika Pahali Patakatifu Sana.


Na nyuma ya pazia lililotenga kile chumba cha kwanza, kulikuwa chumba kingine kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana.


Hivi Roho Mutakatifu alikuwa akionyesha kwamba njia ya kuingia katika Pahali Patakatifu Sana ilikuwa bado kufunguliwa kwa wakati wote ile Hema ya kwanza ilipokuwa ingali ikisimikwa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


Mutatambua Roho wa Mungu kwa njia hii: kila mutu anayesadiki kwamba Yesu Kristo amekuja katika hali ya kimutu yuko na Roho wa Mungu.


Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika dunia. Watu hawa hawakubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili wa kimutu. Yule asiyekubali vile ni mudanganyifu na mupinga Kristo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις