Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.
Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.
Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.
Sisemi hivi kwa kuwaamuru, lakini kwa njia ya kuwaelezea habari za bidii ya wengine, ninataka kuwapima kusudi upendo wenu upate kutambulikana kuwa wa kweli.
Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.
Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.
Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.