Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Nehemia 9:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Kwa sababu ya zambi zetu, utajiri wa inchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kwa kututawala. Wanatutawala jinsi wanavyopenda hata na nyama wetu wa ufugo wanawatendea jinsi wanavyopenda, tuko katika taabu kubwa sana.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Nehemia 9:37
11 Σταυροειδείς Αναφορές  

Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba muji huu ukijengwa upya na kuta zake zikimalizika, watu hawatalipa kodi, malipo ya kuvuka mipaka, na mengine mbalimbali na hazina yako itapunguka.


Zaidi ya hayo, ninatoa amri kwamba ninyi mutawasaidia katika kazi hiyo. Mali zao zote walizotumia zitalipwa bila kuchelewa kutoka katika hazina ya mufalme inayotokana na kodi kutoka katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.


Tunawafahamisha tena kwamba inakatazwa kuwadai kodi ya mapato, malipo ya kuvuka mupaka na mengine makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa mulango, wafanyakazi au watumishi wengine wa nyumba hii ya Mungu.


Nikasema: “Kulingana na uwezo tunaokuwa nao, tumekuwa tukiwanunua tena wandugu zetu Wayuda waliokuwa wameuzishwa kwa watu wa mataifa mengine. Lakini sasa hata munawauzisha wandugu zenu, nasi tunalazimika kuwanunua!” Basi wakanyamaza kimya, bila kuwa na la kujibu.


Tunalazimishwa kufanya kazi kama punda, tumechoka, lakini haturuhusiwi kupumzika.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


Wakamujibu: “Sisi ni wa uzao wa Abrahamu, wala hatujakuwa watumwa wa mutu hata siku moja. Namna gani basi unaweza kutuambia kwamba tutapata uhuru?”


“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,


Mutapanda mizabibu na kuitunza, lakini hamutavuna mizabibu hiyo wala kunywa divai yake, maana wadudu wataikula.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Watakula ngombe wenu na mazao yenu, mpaka muangamie. Hawatawaachia ngano, divai, mafuta, ngombe au kondoo mpaka wawaangamize.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις