Daudi alipokuwa akipita pamoja na watu wake, watu wote katika inchi yote walilia kwa sauti. Mufalme Daudi akavuka kijito cha Kidroni pamoja na watu wote, wakapita kuelekea katika jangwa.
Wakubwa hawakujua pahali nilipokuwa nimekwenda wala nimefanya nini. Tena nilikuwa sijawaambia Wayuda, makuhani, viongozi, wakubwa wala wale watu ambao wangefanya kazi ya kujenga upya muji.
Mulango wa Bonde ukajengwa upya na Hanuni pamoja na wakaaji wa muji wa Zanoa. Wakaweka milango pahali pake, wakatia vyuma na vifungio vyake. Wakajenga upya ukuta ukiwa na urefu wa metre mia ine hivi mpaka kwenye mulango wa Yalala.
Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akaondoka pamoja na wanafunzi wake na kuvuka ngambo ya kijito cha Kidroni. Nao wote wakaingia katika bustani iliyokuwa kule.