Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.
Kwa vile ambavyo hesabu ya makuhani ilikuwa ndogo, hawakuweza kuchuna nyama wale wote. Kwa hiyo, wandugu zao Walawi wakawasaidia mpaka walipomaliza kazi hiyo. Wakati ule, makuhani wengine zaidi walikuwa wamekwisha kujitakasa. (Walawi walijiweka katika hali ya usafi zaidi kuliko makuhani.)
akawaambia: “Munisikilize, enyi Walawi! Mujitakase na mutakase nyumba ya Yawe, Mungu wa babu zenu. Mutoshe uchafu wote unaokuwa katika Pahali Patakatifu.
Waliokula mwana-kondoo wa Pasaka walikuwa Waisraeli wote waliorudi kutoka katika uhamisho pamoja na watu wengine wote ambao walikuwa wameziacha njia za mataifa mengine kwa kumwabudu Yawe, Mungu wa Israeli.
Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.
Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”