Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Nehemia 10:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Kwa kufuata vile ilivyoandikwa katika Sheria kila muzaliwa wa kwanza wa kiume kati ya wana wetu, katika nyumba zetu, atapelekwa katika nyumba ya Mungu wetu kwa makuhani wanaotumika mule, vilevile tutapeleka kila muzaliwa wa kwanza dume wa ngombe zetu, mbuzi zetu na kondoo zetu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Nehemia 10:37
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda, wakaleta vilevile sehemu moja ya kumi ya ngombe na kondoo na ya vitu vitakatifu vilivyotolewa kwa Yawe. Wakaviweka vitu hivyo katika mafungu.


Tena nikagundua kwamba Walawi hawakupewa haki zao; na matokeo yake ni kwamba Walawi na waimbaji waliokuwa wakifanya kazi pale mbele, sasa walikwisha kurudilia mashamba yao.


Kisha, watu wote wa Israeli, wakaanza tena kuleta zaka zao za unga, divai na mafuta kwenye gala.


alimuruhusu Tobia kutumia chumba kikubwa ambamo pale mbele walikuwa wakiweka sadaka za unga, ubani, vyombo, zaka za unga, divai, mafuta; vitu hivyo vyote Waisraeli walivyoagizwa kutoa kwa Walawi, waimbaji, walinzi wa milango, na matoleo kwa makuhani.


Nikaamuru watu, nao wakatakasa vyombo hivyo halafu nikarudisha mule vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka ya unga na ubani.


munapaswa kumuwekea Yawe kila muzaliwa wenu wa kwanza mwanaume. Kila muzaliwa wa kwanza dume wa mifugo yenu atakuwa wa Yawe.


“Unitakasie wazaliwa wote wa kwanza, maana wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli ni wangu, ikuwe wanaume au wanyama.”


Kila jamaa italeta mikate miwili ya sadaka ya kutoa kwa kitambulisho mbele yangu mimi Yawe. Kila mukate utatengenezwa kwa kilo mbili za unga laini uliotiwa chachu na huo mutanitolea mimi Yawe ukiwa ni matoleo ya malimbuko yenu.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.


Kila muzaliwa wa kwanza ambaye Waisraeli watanitolea, akiwa muzaliwa wa kwanza wa wanadamu, au wa nyama, atakuwa wako. Lakini unaweza kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wote wa wanadamu, na kila muzaliwa wa kwanza wa nyama anayekuwa muchafu.


Nyama yao unaweza kuikula, kama vile kilali na muguu wa nyuma wa kuume vinavyotolewa kama vile sadaka ya kutikiswa.


Kuelekea Walawi, hao nimewapa sehemu ya kumi ya kila kitu Waisraeli wanachonitolea kuwa urizi wao. Haya yatakuwa malipo yao kwa kazi wanayotoa katika kulitunza hema la mukutano.


Donge la kwanza la unga wenye kupondwa likitolewa kwa Mungu, mikate itakuwa yake vilevile. Na kama shina la muti likitolewa kwa Mungu, matawi yatakuwa yake vilevile.


“Mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote ya shamba kila mwaka.


Mutawapa sehemu ya kwanza ya mazao yenu ya ngano, divai, mafuta yenu na sufu ya kwanza ya kondoo wenu.


utatwaa malimbuko ya mazao utakayovuna katika inchi Yawe, Mungu wenu, anayokupa, na kuyaweka katika kikapu mpaka pale pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, amechagua pawe makao yake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις