Yuda akamwambia baba yake Israeli: “Uniruhusu mimi niende naye kusudi tuondoke mara moja, tuende tununue chakula, tusikufe na njaa pamoja nawe na watoto wetu.
“Basi, mufanye haraka! Muende kwa baba na kumwambia: ‘Mwana wako Yosefu anasema: Mungu amenifanya kuwa mukubwa wa inchi yote ya Misri. Basi, usikawie kuja kwangu.
Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.
Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Mutu hawezi kuishi kwa mukate tu, lakini kwa njia ya kushika kila neno Mungu analosema.’ ”