Basi, Yakobo akainua macho, akamwona Esau akikuja pamoja na watu mia ine. Halafu, akawagawanya watoto wake kati ya Lea, Rakeli na wale wajakazi wawili.
Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba, halafu anakutana na dubu! Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake, na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka.
sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.
Hao wajumbe walikwenda, kisha wakarudi na kumwambia Yakobo: “Tumefika kwa ndugu yako Esau, naye yuko katika njia kuja kukupokea, akiwa na watu mia ine.”
Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”
Esau akasema: “Heri nikuachie sehemu ya watu wangu.” Lakini Yakobo akasema: “Kuna sababu gani ya kufanya hivyo? Inanitosha kwamba mimi nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe bwana wangu.”
Siku moja, Ruta wa Moabu akamwambia Naomi: “Muniruhusu niende kukusanya masalio ya mavuno pahali nitakapopata kukubaliwa na mwenye shamba.” Naomi akamwambia: “Basi, uende binti yangu.”
Ruta akamujibu: “Bwana, wewe umenifanyia wema mukubwa sana. Ingawa mimi si kama mumoja wa watumishi wako, nimetosheka kwa sababu umenifariji sana na kuongea nami kwa upendo.”