Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mwanzo 32:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wewe uliniahidi kunitendea mema na kuwafanya wazao wangu wakuwe wengi kama muchanga wa bahari ambao hauhesabiki kwa wingi wake.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mwanzo 32:13
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.


Zawadi inamufungulia mutu milango; inaweza kumufikisha mutu mbele ya mukubwa.


Hasira inatulizwa kwa zawadi ya siri; kituliro kinachotolewa kwa uficho kinatuliza kasirani.


Watu wengi wanajipendekeza kwa wakubwa; kila mutu anataka kuwa rafiki wa mutu mwenye kupana.


Kwa anayetoa kituliro ni kama hirizi; kila kitu anachofanya yeye anafanikiwa.


Yosefu, aliporudi kwake, wakamuletea zile zawadi walizokuwa nazo, wakainama mbele yake kwa heshima.


Bwana wangu, ninakuomba upokee zawadi hii niliyokuletea, na uwape vijana wanaokufuata.


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.


Yakobo akamwambia: “Hapana! Kama kweli nimekubaliwa mbele yako, ninakusihi uipokee zawadi yangu. Hakika, kuona uso wako ni kama kuona uso wa Mungu, kwa vile ulivyonipokea kwa wema mukubwa.


Alipoinua macho yake, akaona watu watatu wakisimama mbali kidogo mbele yake. Mara tu alipowaona, akakimbia kutoka kwenye mulango wa hema yake, akakwenda kuwapokea. Alipowafikia akainama kwa heshima


Basi, Yakobo akalala pale usiku ule. Kisha akatenga sehemu ya mali yake, ikuwe zawadi kwa ndugu yake Esau:


Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”


Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!


Yawe akamupeleka Abramu inje na kumwambia: “Angalia mbinguni! Uhesabu nyota, kama kweli utaweza kuzihesabu! Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi!”


hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao.


Nikawaambia wakubwa, wasimamizi na watu wote kwa jumla: “Kazi ni kubwa, na kuna hatua kubwa kati ya mutu na mwenzake juu ya ukuta.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις