Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.
Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.
Utasema nini juu ya wale uliowazoeza kuwa warafiki zako, wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha, watakapokushinda na kukutawala? Si utashikwa na uchungu sawa vile mwanamuke anayezaa?
Enyi wakaaji wote wa Lebanoni, ninyi munaokaa salama kati ya miti ya mierezi, mutaugua sana wakati mutakaposhikwa na uchungu unaokuwa kama wa mwanamuke anayezaa!
Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!
Lakini kama mume wake atakaposikia habari zake, akizifunga na kuzivunja, basi, hata kama alitaka kutimiza kiapo au ahadi zake, hataombwa kuzitimiza. Mume wake atakuwa amezifunga na Yawe atamusamehe.
Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.
Muke hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa mume wake. Vilevile mume hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa muke wake.
Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.