Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mwanzo 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha akamwambia mwanamuke: “Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa, Utazaa watoto kwa uchungu. Utakuwa na hamu na mume wako, naye atakutawala.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mwanzo 3:16
30 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”


Kulikuwa mutu mumoja jina lake Yabesi, aliyeheshimiwa kuliko wandugu zake wote. Mama yake alimupa jina la Yebesi kwa sababu alizaa kwa maumivu.


Amri hiyo itakapotangazwa katika eneo lote la utawala wako, kila mwanamuke atamuheshimu mume wake, akuwe tajiri au masikini.”


Lakini walipouona Sayuni, wakashangaa; wakashikwa na hofu na kukimbia.


Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.


Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Utasema nini juu ya wale uliowazoeza kuwa warafiki zako, wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha, watakapokushinda na kukutawala? Si utashikwa na uchungu sawa vile mwanamuke anayezaa?


Enyi wakaaji wote wa Lebanoni, ninyi munaokaa salama kati ya miti ya mierezi, mutaugua sana wakati mutakaposhikwa na uchungu unaokuwa kama wa mwanamuke anayezaa!


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Watu wa Damasiki wamevunjika moyo; wamegeuka kusudi wapate kukimbia; hofu kubwa imewashika, uchungu na huzuni vimewapata, kama mwanamuke anayezaa.


Waisraeli wanasema: Tumesikia habari zao. Kwa hiyo mikono yetu imeregea; tumeshikwa na huzuni na uchungu, kama mwanamuke anayezaa.


Lakini kama mume wake atakaposikia habari zake, akizifunga na kuzivunja, basi, hata kama alitaka kutimiza kiapo au ahadi zake, hataombwa kuzitimiza. Mume wake atakuwa amezifunga na Yawe atamusamehe.


Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.


Lakini ninataka mufahamu maneno haya: Kristo ni kichwa cha kila mwanaume, na mwanaume ni kichwa cha muke wake, na Mungu ni kichwa cha Kristo.


wanawake wanapaswa kukaa kimya katika mikutano ya kanisa. Wao hawaruhusiwi kusema katika kanisa, lakini wanapaswa kutii sawa vile Sheria inavyosema.


Muke hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa mume wake. Vilevile mume hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa muke wake.


Wake muwatii waume wenu kama vile inavyostahili mbele ya Bwana.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Kwa maana, Adamu ndiye aliyeumbwa wa kwanza, na kisha Eva.


Ingawa hivi mwanamuke ataokolewa kwa kuzaa watoto, kama akidumu katika imani, upendo na utakatifu na kuwa mukadirifu.


na kuwa wenye utaratibu, wenye maisha safi, wenye kutunza nyumba zao vizuri, wema na wenye kutii waume wao, kusudi Neno la Mungu lisitukaniwe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις