Watu wa kule walipomwuliza juu ya muke wake, akajibu: “Huyu ni dada yangu.” Aliogopa kusema kwamba ni muke wake kwa kuogopa kwamba wakaaji wa inchi wangemwua kwa sababu ya Rebeka, maana Rebeka alikuwa muzuri sana.
Abimeleki akamwita Isaka na kumwambia: “Hakika huyo ni muke wako! Sababu gani ulisema kwamba ni dada yako?” Isaka akajibu: “Kwa sababu niliogopa kwamba ningeuawa kwa sababu yake.”
Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua.
Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.
“Mama ya Sisera akaangalia toka kwenye dirisha, akachungulia, kisha akalalamika: ‘Kwa nini gari lake limechelewa? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa kusikilika?’