18 Simama umwinue mutoto na kumushika vizuri katika mikono yako, maana nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa.”
Na juu ya huyo mwana wa mujakazi wako nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa kwa sababu yeye vilevile ni mutoto wako.”
Zaidi ya hayo, malaika wa Yawe akamwambia Hagari: “Nitawazidisha wazao wako hata wasiweze kuhesabika kwa wingi wao.”
“Na juu ya Isimaeli, nimesikia ombi lako. Nitamubariki, nitamujalia watoto wengi na kuwazidisha sana. Isimaeli atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamufanya kuwa baba wa taifa kubwa.
Malaika wa Yawe akamukuta Hagari kwenye chemichemi ya maji katika jangwa, chemichemi iliyokuwa katika njia kuelekea Suri.
Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”