Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mwanzo 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Yawe Mungu akamwamuru yule mwanaume: “Unaweza kula matunda ya muti wowote katika bustani.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mwanzo 2:16
8 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha Mungu akasema: “Ninawapa kila mumea katika dunia unaozaa mbegu na kila muti unaozaa matunda yenye mbegu, kwa ajili ya chakula chenu.


Basi, Yawe Mungu akamutwaa yule mwanaume, akamuweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.


Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya.


lakini Mungu alisema: ‘Musikule matunda ya muti unaokuwa katikati ya bustani, wala musiuguse. Kama sivyo, mutakufa.’ ”


Kila kitu Mungu alichokiumba ni kizuri, wala hakuna kile kinachopaswa kukataliwa, lakini inafaa kumushukuru Mungu mbele ya kukikula.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις