Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”
Alifanya hivyo kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi hata wasiweze kuishi pamoja. Inchi walimokaa kama wageni haikuweza kuwatoshelea kwa sababu ya wingi wa nyama wao.
Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.
Musa akaendelea kuwaambia watu: “Vilevile, wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana na kuwapa inchi ile kama vile alivyowaapia ninyi na babu zenu,
basi, bwana wake atamuleta mbele ya Mungu. Kisha atamupeleka kwenye mulango au kwenye kizingiti na kumutoboa sikio lake kwa chuma chenye kuchongwa. Naye atamutumikia bwana wake maisha yake yote.
Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.
Kisha uwapakae mafuta kama vile ulivyomupakaa baba yao, kusudi nao vilevile wanitumikie kama makuhani. Kupakwa mafuta huku kutawaingiza katika ukuhani wa kudumu katika vizazi vyao vyote.
Wao waliwaambia hivi: Kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu na matendo yake mabaya, kusudi mupate kuishi katika inchi ambayo Yawe amewapa ninyi na babu zenu tangu zamani kuwa urizi wenu milele.
Wewe mwanadamu! Wakaaji waliobaki katika miji iliyoharibiwa katika inchi ya Israeli wanasema: Abrahamu alikuwa peke yake, hata hivyo, alipata kurizi inchi hii. Lakini sisi ni wengi; ni wazi tumepewa inchi hii ikuwe yetu!
Mutakapoingia katika inchi ya Kanana ambayo ninawapa kuwa urizi wenu, nami nikifanya namna ya ukoma uote katika ukuta wa nyumba fulani katika inchi mutakayorizi,
Hili ni sharti la kufuata siku zote. Linapaswa kufuatwa kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya watu wa Israeli mara moja kila mwaka na kusamehewa zambi zao. Musa akafanya yote kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
Musa akamwambia shemeki yake Hobabu mwana wa Reueli Mumidiani, baba mukwe wake: Sisi tunasafiri kwenda pahali ambapo Yawe amesema: Nitawapa ninyi pahali hapo. Basi, tuende pamoja, nasi tutakutendea vizuri maana Yawe ameahidi kutendea Waisraeli vizuri.
Ninaagana naye kwamba yeye na wazao wake watakuwa makuhani milele kwa sababu aliona wivu kwa ajili yangu mimi Mungu wake, akawafanyia Waisraeli upatanisho.
Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.
“Panda juu ya mulima huu wa Abarimu, mulima Nebo katika inchi ya Moabu, kuelekea muji wa Yeriko, uiangalie inchi ya Kanana ninayowapa Waisraeli wairizi.
Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”
Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.
Kwa sababu hii, Kristo ni mupatanishi wa agano jipya. Kwa njia ya kufa kwake aliwakomboa watu toka katika makosa waliyofanya chini ya uongozi wa agano la kwanza, kusudi wale walioalikwa na Mungu wapate kupokea urizi wa milele aliowaahidia.