Kisha, Sarai akamupa Abramu Hagari, mujakazi wake Mumisri, akuwe muke wake. Haya yalitokea nyuma ya Abramu kukaa katika inchi ya Kanana kwa muda wa miaka kumi.
Sarai akamwambia Abramu: “Lazima ya ubaya ninaotendewa ikuwe juu yako. Mimi nilikupa mujakazi wangu, lakini alipopata mimba, mimi nimekuwa kitu bure mbele ya macho yake! Yawe ahukumu kati yako na mimi!”
Sanduku la Yawe lilipokuwa linaingia katika muji wa Daudi, Mikali binti wa Saulo alichungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele ya Yawe. Basi, akamuzarau ndani ya moyo wake.
Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.