Kule, walipata malisho tele, tena mazuri sana na tena inchi ilikuwa wazi, tulivu na yenye amani, maana wenyeji wa inchi hiyo wa zamani walikuwa wazao wa Hamu.
Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
Musonge mbele, enyi farasi; mushambulie, enyi magari ya vita. Mashujaa wasonge mbele: watu wa Etiopia na Puti wanaoshika ngao, watu wa Ludi, wafundi wa kutumia pinde.
Watu kutoka Persia, Ludi na Puti walijiunga katika kundi lako la waaskari; walilundika ngao zao na kofia zao kwenye kambi zao za kiaskari. Waaskari hao walikupatia utukufu.