Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 6:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Yawe atapendezwa nikimutolea maelfu ya kondoo dume, au mito elfu na elfu ya mafuta? Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, mutoto wangu wa kwanza kwa ajili ya zambi yangu?

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 6:7
29 Σταυροειδείς Αναφορές  

lakini alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli. Akamutambikia hata mwana wake kwa kuteketezwa kwa moto, akifuata desturi mbaya za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipoitwa Tofeti katika bonde la wana wa Hinomu, kusudi mutu yeyote asimuteketeze mwana wake au binti yake kama sadaka kwa Moleki.


Hapo akamutwaa mwana wake wa kwanza ambaye angekuwa mufalme kwa pahali pake, akamutoa kuwa sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta wa muji. Watu wa Israeli walipoona hayo, wakachukizwa sana. Wakauacha muji ule na kurudia katika inchi yao.


Nyakati hizo niliogelea kwenye fanaka. Mawe yalinitiririshia vijito vya mafuta.


Kwa kweli sihitaji ngombe dume wa zizi lako, wala beberu wa nyumba yako,


Uniokoe kutoka kosa la kumwanga damu, ee Mungu, Mungu mwokozi wangu, nami nitaimba kwa sauti kwamba umeniokoa.


Kweli wewe haupendezwi na sadaka. Hautaki nikutolee sadaka za kuteketezwa.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Kuni zote za Lebanoni na nyama wake wote havitoshi kwa sadaka ya kuteketezwa mbele yake.


wanamujengea mungu Bali mazabahu, kwa kusudi la kuwachoma wana wao kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya mungu yule. Mimi sikuwaamuru hata kidogo kufanya vile, wala halikunifikia katika roho.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Wamejenga mazabahu inayoitwa “Tofeti” huko kwenye bonde la Mwana wa Hinomu, kwa kuwatolea wana na wabinti kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Mimi sikukuwa nimewaamuru kufanya jambo hilo, wala halikunifikia katika mafikiri.


Wamefanya uzinzi na mauaji. Wamefanya ukahaba kwa sanamu zao, hata kuzitambikia watoto walionizalia wao wenyewe.


Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ngombe, kumutafuta Yawe; lakini hawataweza kumupata, kwa sababu amejitenga nao.


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Usimutoe mutoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utazarau jina langu mimi Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Hata mukinitolea sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na za vyakula, mimi sitakubali kuzipokea; na sadaka zenu za amani za nyama wanono mimi sitaziangalia kabisa.


Sasa ninamurudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.


basi, yeyote atakayetoka inje kutoka katika nyumba yangu kuja kunipokea nitakapokuwa ninarudi nyuma ya kuwashinda Waamoni, huyo atakuwa wako wewe Yawe. Nitakutolea kama sadaka ya kuteketezwa.”


Nyuma ya miezi miwili akarudi kwao. Kisha baba yake akamutendea kulingana na kiapo chake. Binti huyo hakukuwa amemujua mwanaume yeyote. Basi, tangu wakati ule kukakuwa desturi hii katika Israeli:


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις