Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 6:5
37 Σταυροειδείς Αναφορές  

Amesababisha matendo yake ya ajabu yakumbukwe; Yawe ni mwenye huruma na rehema.


Ulinde uzima wangu, ee Yawe, kwa ajili ya jina lako, uniondoe katika taabu, kwa ajili ya haki yako.


Wewe ndiwe asili ya uzima; kwa mwangaza wako tunaona mwangaza.


Nguvu na haki yako, ee Mungu, vinafika mpaka juu katika mbingu. Wewe umefanya mambo makubwa sana. Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe?


Muji Sayuni utakombolewa kwa njia ya kufuata sheria ya Mungu, nao wakaaji wake waliogeuka toka zambi zao kwa njia ya haki.


Kesho yake, Balaki akamutwaa Balamu, akapanda naye mpaka Bamoti-Bali; kutoka huko, Balamu aliweza kuwaona wamoja kati ya Waisraeli.


Balaki akamwambia Balamu: Kuja, nitakupeleka pahali pengine. Labda Mungu atakubali uwalaani watu hao kutoka huko kwa ajili yangu.


Waisraeli walipokuwa kule Sitimu, wanaume wakaanza kuzini na wanawake wa Moabu.


Wanawake hao waliwaalika Waisraeli washiriki matambiko waliyotambikia miungu yao, nao Waisraeli wakakula chakula na kuabudu miungu yao.


Mukumbuke kwamba wanawake ndio waliofuata shauri la Balamu, wakasababisha Waisraeli wamwasi Yawe kule Peori hata ugonjwa mukali ukawafikia watu wa Yawe.


Kati ya watu hao waliouawa, kulikuwa wafalme watano wa Midiani: Ewi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile wakamwua Balamu mwana wa Beori.


Wakapiga kambi hiyo karibu na muto Yordani kati ya Beti-Yesimoti na bonde la Abeli-Sitimu kwenye mabonde ya Moabu.


Basi mukumbuke namna mulivyokuwa zamani ninyi munaokuwa kwa kizalikio watu wa mataifa mengine. Wayuda wanawaita ninyi watu wasiotahiriwa, lakini wao wanajiita wenye kutahiriwa kwa sababu ya kitambulisho cha kutahiriwa na watu katika miili yao.


Musikule sadaka hiyo na mikate iliyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso – kwa sababu mulitoka Misri kwa haraka; kwa hiyo, muda wote mutakaoishi mutakumbuka ile siku mulipotoka Misri.


Lakini Yawe, Mungu wenu, hakumusikiliza Balamu; pahali pake laana hiyo iligeuka kuwa baraka, kwa sababu Yawe, Mungu wenu, aliwapenda.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


“Mukumbuke na musisahau jinsi mulivyomukasirikisha Yawe, Mungu wenu, kule katika jangwa. Tangu siku ile mulipotoka katika inchi ya Misri mpaka siku mulipofika pahali hapa, ninyi mumekuwa mukimwasi Yawe.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.


Asubui mapema Yoshua pamoja na watu wote wa Israeli walianza safari kutoka Sitimu. Walipofika kwa muto Yordani, walipiga kambi hapo kwa muda mbele ya kuvuka.


Waisraeli walivuka muto Yordani katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, wakapiga kambi kule katika muji wa Gilgali, upande wa mashariki wa Yeriko.


Wameacha njia ya kweli na kupotoka wakifuata njia ile Balama, mwana wa Beori, aliyofuata. Huyu alipenda kupata mali kwa njia isiyokuwa ya haki,


Lakini tukiitikia zambi zetu mbele ya Mungu, yeye atatusamehe zambi zetu na kutusafisha toka katika maovu yote kwa maana yeye ni mwaminifu na mwenye haki.


Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


Unazani wewe una nguvu kuliko Balaki mwana wa Sipori aliyekuwa mufalme wa Moabu? Yeye hakushindana na Waisraeli au kupigana nao.


Kwenye visima vya maji, tangaza ushindi wa Yawe, ushindi kwa walimaji wake katika Israeli. Watu wa Yawe walishuka kwenye mulango wa muji.


Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις