Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 6:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 6:4
29 Σταυροειδείς Αναφορές  

Tena, hakuna watu katika dunia ambao wanaweza kufananishwa na watu wako Waisraeli. Ulikwenda kuwakomboa kutoka Misri na miungu yake kusudi wakuwe watu wako. Ukawafanyia jina na kuwatendea mambo makubwa na ya ajabu.


Wewe ukajifanyia njia juu ya bahari; ulitembea juu ya maji yale mengi, lakini pahali ulipopita hapakuonekana.


Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Sasa, nitakutuma kwa mufalme wa Misri kusudi uwatoe watu wangu, watu wale wa Israeli, kutoka katika inchi ya Misri.”


Lakini Musa akamwambia Yawe: “Ewe Bwana wangu, mimi mutumishi wako sina ufundi wa kusema tangu zamani, hata kisha kusema nawe. Ulimi wangu ni muzito.”


Haruni ataongea na Waisraeli kwa ajili yako. Yeye atakuwa musemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.


Ndio haohao Musa na Haruni walioongea na mufalme wa Misri, juu ya kuwatoa Waisraeli kutoka inchi ya Misri.


Kwa maajabu na miujiza uliyowatisha nayo Wamisri, uliwatoa watu wako Misri kwa nguvu zako nyingi na uwezo wako mukubwa.


Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


Kisha Miriamu na Haruni wakaanza kumusema Musa vibaya kwa sababu ya mwanamuke Mukushi aliyekuwa amemwoa.


Hivi ndivyo vituo ambavyo Waisraeli wakapiga kambi walipotoka Misri wakiwa katika makundi ya makabila yao chini ya uongozi wa Musa na Haruni.


Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa katika inchi ya Misri, na Yawe, Mungu wenu, akawakomboa kutoka huko. Kwa hiyo ninawapa amri hiyo.


Lakini ninyi ndio watu aliowakomboa kutoka Misri katika furu la chuma. Aliwatoa huko kusudi mukuwe watu wake kama vile munavyokuwa hivi leo.


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Lakini ni kwa sababu Yawe anawapenda na anashika kiapo alichowaapia babu zenu, ndiyo maana aliwaokoa kwa nguvu zake kubwa na kuwaokoa toka katika utumwa, toka mikono ya mufalme wa Misri.


Nikamwomba Yawe, nikisema: Ee Yawe, usiwaangamize watu wako na urizi wako, watu uliowakomboa na kuwatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo na nguvu yako kubwa.


Samweli akawaambia: “Yawe ndiye aliyemuchagua Musa na Haruni na kuwaondoa babu zenu katika inchi ya Misri.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις