Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wakati unakuja ambapo mutamulilia Yawe, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mumetenda mambo maovu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 3:4
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakati atakapopatwa na taabu, Mungu atasikia kilio chake?


Kweli Mungu hasikilizi kilio cha bure; Mungu Mwenye Uwezo hajali kilio kile.


Uliwakimbiza waadui zangu, na wale walionichukia niliwaangamiza.


Halafu mutaniita lakini sitaitika; mutanitafuta kwa bidii lakini hamutanipata.


Anayekataa kuisikia sheria, yule, hata maombi yake, ni chukizo kwa Mungu.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Nitaleta hasara juu yao ambayo hawataweza kuiepuka. Hata kama wakinililia namna gani, sitawasikiliza.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Watu watajaribu kupigana na Wakaldea lakini hiyo itakuwa bure, maana mifereji itajaa maiti za watu ambao nitawaua kwa hasira na kasirani yangu. Kwa vile wamefanya uovu huo wote, mimi nitauacha muji huu.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.


Waonaji watafezeheka, waaguzi watapata haya; wote watafunga midomo yao, maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.


Lakini inchi yote nyingine itakuwa jangwa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


nikasema: Kwa sababu niliwaita nao hawakunisikiliza, basi, nao waliponiita, sikuwasikiliza.


Siku ile ya hukumu itakapotimia, wengi wataniambia: ‘Bwana, Bwana, sisi hatukutangaza ujumbe wa Mungu? Nasi hatukufukuza pepo kwa jina lako na kufanya maajabu mengi kwa jina lako?’


“Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’


Tunajua kwamba Mungu hasikilizi maombi ya wenye zambi, lakini anamusikiliza mutu yule anayemuheshimu na kufanya sawa anavyotaka.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Wakati huo, ninyi mutalalamika kwa sababu ya mufalme wenu ambaye mumejichagulia ninyi wenyewe. Lakini Yawe hatawajibu.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις