Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini Yawe anawaambia ninyi hivi: Munawatendea watu wangu kama adui. Munawanyanganya watu watulivu nguo zao; watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi, na wasiokuwa na mafikiri yoyote ya vita.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 2:8
10 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mimi ni mumoja wa wale wanaopenda amani na uaminifu katika Israeli. Sasa wewe unakusudia kuuharibu muji ambao ni sawa vile katika Israeli. Kwa nini sasa unataka kuuangamiza muji unaokuwa mali ya Yawe?”


Mungu anayetawala tangu milele, atanisikia na kuwafezehesha waadui yangu, maana hawapendi kubadilika, wala hawamwogopi Mungu.


Wachaguliwa wangu wamenigeuka, wamekuwa kama simba katika pori, wameningurumia mimi; ndiyo maana ninawachukia.


Lakini ninyi munachukia mazuri na kupenda mabaya. Munawachuna ngozi watu wangu, na kunyofoa nyama juu ya mifupa yao.


Munajikulisha kwa nyama ya watu wangu, munawachuna ngozi yao, munaivunjavunja mifupa yao, na kuwakatakata kama nyama ya kupika, kama nyama ya kutia ndani ya chungu.


Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις