Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kama mutu angetokea akitangaza maneno matupu ya uongo na kusema “Ninawatabiria divai na pombe kwa wingi”, muhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 2:11
35 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yule muzee wa Beteli akamwambia: “Mimi vilevile ni nabii kama wewe, na Yawe amesema nami kwa njia ya malaika akisema: ‘Umurudishe kwako, akule chakula na kunywa maji.’ ” Lakini yule nabii muzee alikuwa anamudanganya tu.


Basi, Ahabu akakusanya manabii yapata mia ine, akawauliza: “Niende au nisiende kushambulia Ramoti-Gileadi?” Nao wakamujibu: “Kwenda! Yawe atakupatia ushindi.”


Mungu anipime katika mizani ya haki, naye ataona kwamba sina kosa. Kama nimeishi kwa kufuata uongo, kama nimekimbilia kudanganya watu,


Kama vile mawingu na upepo bila mvua, ndivyo anavyokuwa mutu anayeahidi zawadi na haitoi.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha, na hao wanaoongozwa nao wamepotoka.


Naye Yawe akaniambia: Hao manabii wanatoa unabii wa uongo kwa jina langu. Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi yao hayana maana yoyote, wao wanajitungia uongo wenyewe.


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Wanawaambia hivi wale wanaozarau neno langu mimi Yawe: Mambo yenu yataendelea vizuri. Na wanamwambia hivi kila mutu anayefuata ugumu wa moyo wake na mawazo yake: Hakuna hasara yoyote itakayokupata!


Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema: Nimeota ndoto, nimeota ndoto!


Vilevile mimi Yawe ninasema kwamba nitawashambulia manabii wanaotabiri ndoto zao za uongo kwa watu wangu, na kuwapotosha kwa uongo wao na upuuzi wao. Mimi sikuwatuma wala kuwaamuru waende, kwa hiyo hawatawafalia watu hao kitu. –Ni ujumbe wa Yawe!


Basi, nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania: Sikiliza, Hanania. Yawe hakukutuma, nawe unawafanya watu hawa waamini uongo.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu. Hawakufichua wazi uovu wako kusudi wapate kukurudishia hali yako ya mbele. Lakini walikuonea maono ya uongo na ya kupotosha.


Kwa sababu mumewavunja watu wa haki moyo kwa kusema uongo, ijapokuwa mimi sikuwavunja moyo, mukawaimarisha waovu wasiache mienendo yao mibaya na kuokoa maisha yao,


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


Yawe anasema hivi juu ya manabii wanaowapotosha watu wake, manabii ambao wanatabiri amani wakipewa kitu, lakini wanawatishia watu kwa vita wasipopewa kitu:


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις