Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mika 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Enyi watu wa Yuda, munyoe vichwa vyenu kwa kuwaomboleza watoto wenu wapenzi; mupanue upaa wenu ukuwe mupana kama wa tai, maana watoto wenu watawaacha kwenda katika uhamisho.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mika 1:16
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Kisha Yobu akasimama, akapasua nguo yake, akanyoa nywele zake, akajitupa chini na kumwabudu Mungu,


Watu wa Diboni wamepanda katika hekalu pahali pa juu kwa kuomboleza, watu wa Moabu wanalia kwa ajili ya Nebo na Medeba; vichwa vyote vimenyolewa upaa, ndevu zao zote zimekatwa kabisa.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Wote, wakubwa kama vile wadogo, watakufa katika inchi hii; nao hawatazikwa, wala hakuna atakayeomboleza juu yao. Hakuna atakayejikatakata wala kunyolewa upaa kwa ajili ya kifo chao.


Kwa hiyo, muvae gunia, muomboleze na kulia; kwa maana Yawe hajaondoa hasira yake kali kwenu.


Watu wa Gaza wamenyoa kichwa kwa kuomboleza; muji wa Askeloni umeangamia. Enyi watu muliobaki katika bonde mutajikatakata kwa huzuni mpaka wakati gani?


Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.


Munyoe nywele zenu na kuzitupa, enyi wakaaji wa Yerusalema: mufanye maombolezo juu ya vichwa vya milima, maana, mimi Yawe nimewakataa ninyi, nimewatupilia ninyi kizazi kilichosababisha hasira yangu!


Usiku kucha uamukeamuke na kulia. Umufungulie Yawe yanayokuwa ndani ya moyo wako. Umwinulie mikono yako kwa kuwaombea watoto wako, watoto wanazimia na njaa popote katika barabara.


Anachosema ni hiki: Yeroboamu atakufa kwa upanga nao Waisraeli watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Muke wako atakuwa kahaba katika muji, na wana wako na wabinti zako watauawa katika vita. Inchi yako itagawanywa na kupewa wengine, nawe mwenyewe utakufia katika inchi inayohesabiwa kuwa chafu; nao Waisraeli hakika watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Mutazaa watoto wanaume na wanawake, lakini hawatakuwa wenu, watapelekwa katika uhamisho.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις