Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mezali 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kwa hiyo gala zako zitajaa ngano, na mitungi yako itafurika na divai mupya.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mezali 3:10
15 Σταυροειδείς Αναφορές  

Azaria, Kuhani Mukubwa aliyekuwa wa uzao wa Sadoki akamujibu: “Tangu wakati watu walipoanza kuleta matoleo yao katika hekalu, tumekuwa na vyakula vya kutosha na hata tuna akiba kubwa. Yawe amewabariki watu wake, ndiyo maana tumepata vitu hivi vyote.”


Kila kazi aliyoifanya katika utumishi wa nyumba ya Mungu au katika kutii sheria na amri za Mungu kwa kufuata uongozi kutoka kwake, alizifanya kwa moyo wake wote, naye akafanikiwa.


Gala zetu zijae mavuno ya kila aina. Kondoo wetu katika mbuga wazae maelfu na maelfu.


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia atabarikiwa, maana anagawanya chakula chake na masikini.


Nafasi ya kupepetea itajaa ngano, vikamulio vitafurika divai na mafuta.


Ingawa sasa hakuna ngano ndani ya gala, nayo mizabibu, tini, mikomamanga na mizeituni haijazaa kitu, lakini tangu leo, nitawabariki.


Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”


Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.


Baraka za Yawe zitakuwa katika gala zenu za ngano na katika shuguli zenu zote. Atawabariki katika inchi ambayo anawapa.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις