Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Mezali 10:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Mezali 10:4
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mipango ya mutu wa bidii inaleta mali kwa wingi, lakini kila mutu anayetenda kwa harakaharaka anapata umasikini.


Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.


Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.


Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


Usipende usingizi usikuje kuwa masikini; ukuwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.


Muvivu anatia mukono wake katika sahani lakini hauinui mpaka kwenye midomo.


Kuwa na bidii kutamupa mutu cheo, lakini uvivu utamufanya mutumwa.


Kuna watu wanaotoa mali yao kwa wingi na kuzidi; lakini wachoyo wanazilinda na kuendelea katika umasikini.


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


Kutokana na uvivu wa mutu, paa ya nyumba inaanguka; kwa sababu ya uregevu, nyumba inavuja.


Mwenye akili anakusanya wakati wa mavuno. Kulala wakati wa kuvuna ni haya.


Mwindaji muvivu hatapata anachowinda, lakini mwenye bidii atafanikiwa.


Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.


Siku ileile watumishi wa Isaka walimufikia na kumupasha habari za kile kisima walichokuwa wamechimba, wakasema: “Tumepata maji!”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις