18 Wao wanavizia na kujiangamiza wao wenyewe, wanatega mutego wa kujinasa wao wenyewe.
Mataifa yameanguka katika shimo walilochimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliotega.
Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.
Mutu anayelemewa na kosa ya kuua mutu, atakuwa mukimbizi mpaka katika kaburi. Mutu yeyote asijaribu kumusaidia.
Utue muzigo wako kwa Yawe, naye atakusaidia; hamwachilii mutu wa haki ashindwe.
Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.
Wakisema: “Twende kuvizia mutu na kumwua; kuja tuwashambulie wasiokuwa na kosa!
Mutego unaotegwa na ndege akiona, mutego ule unategwa bure.
Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.
Haki ya watu wakamilifu inanyoosha njia yao, lakini waovu wanaanguka kwa uovu wao wenyewe.