“Muti ukiwa muzuri, matunda yake yatakuwa mazuri vilevile; nao muti ukiwa mubaya, matunda yake yatakuwa mabaya vilevile. Kwa maana muti unatambulikana kwa matunda yake.
Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”
Wandugu zangu, muti unaotoa matunda ya tini unaweza kutoa matunda ya muzeituni? Au muzabibu unaweza kutoa matunda ya tini? Hapana! Hivi vilevile kisima kinachotoa maji ya chumvi hakiwezi kutoa maji matamu.