Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Matayo 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu alipomaliza kutoa maagizo hayo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, akaondoka kule, akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji ya inchi ile.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Matayo 11:1
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, makundi ya watu wakashangaa sana kwa kuona namna alivyowafundisha;


Yesu alizunguka katika miji na vijiji vyote, akiwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, akiwahubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Basi wanafunzi wakaondoka, wakahubiri watu kwamba wageuke toka zambi zao.


Lakini wakazidi kusema kwa nguvu: “Kwa njia ya mafundisho yake anawashawishi watu kufanya uasi katika Yudea yote. Alianzia Galilaya na sasa amefika hapa.”


Nyuma ya pale Yesu akapita katika miji na vijiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza Habari Njema ya Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walienda naye


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Akatuagiza kutangaza Habari Njema kwa watu na kushuhudia kwamba ni yeye aliyewekwa na Mungu kuwa Mwamuzi wa wazima na wafu.


Kwa maana munajua maagizo gani tuliyowatolea kutoka kwa Bwana Yesu.


Kwa maana, wakati tulipokuwa kwenu, tulikuwa tunawaagiza hivi: “Mutu yeyote asiyetaka kutumika, na hapaswi kula vilevile.”


Wandugu, tunawaagiza katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba mujitenge na wandugu wote wanaokuwa wavivu na wasiofuata mafundisho tuliyowapa.


ushike mambo uliyoagizwa kwa uaminifu bila kosa mpaka Siku Bwana wetu Yesu Kristo atakapotokea.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις