Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Yesu alizunguka katika miji na vijiji vyote, akiwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, akiwahubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Lakini wakazidi kusema kwa nguvu: “Kwa njia ya mafundisho yake anawashawishi watu kufanya uasi katika Yudea yote. Alianzia Galilaya na sasa amefika hapa.”
Nyuma ya pale Yesu akapita katika miji na vijiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza Habari Njema ya Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walienda naye
mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.
Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.